Hatimaje siku za hivi Karibuni msanii maarufu wa kike wa filamu za Kibongo Aunt Ezekiel ameonekana akiwa ndani ya shela a.k.a gauni la harusi, hali hiyo imezua maswali mengi kwa baadhi ya watu baada ya msanii huyo kufunga ndoa na kutopatikana kwa taarifa za kuachika kwake na mume wa kwanza .
Mnyetishaji wa habari hii amesema ,nilikutana na Aunt maeneo ya Afrika sana akitoka kwenye saloon moja ijulikanayo kama Wedding Dover. Hali hii imeleta sintofahamu na watu wengi wameamini alikuwa akielekea ukumbini.
Wadaku wa mjini wamedai Mbaby huyo kafunga ndoa ya siri na mzazi mwenzake Moses aka Iyobo, inasemakana Aunt alifuatwa na baadhi ya wanahabari na kutaka kujua yaliyojili kwa bahati mbaya hakuwa muwazi ila alisema "Muda utakapofika nitaweka wazi kila kitu... “Unajua kila mtu katika maisha yake na taratibu zake, sasa mimi bado sijapanga kulizungumzia hilo la kufunga ndoa ya siri mimi na Iyobo. Ila muda ukifika nitaweka wazi kila kitu. Hilo gauni lisikutishe ndugu yangu,” alisema Aunt.
Stay tune......................
No comments:
Post a Comment