Baada ya habari kuzagaa mjini kuwa mastaa wa filamu za Kibongo, Wastara Juma na Bond Suleiman kurudiana , kumeibuka habari mpya zinazodai kuwa watoto wa Wastara hawakupenda mama yao kufunga ndoa na mwanaume mwingine zaidi ya BOND....
Wastara baada ya uvumi wa kuwa na mahusiano na Bond na kuachana kwao kwenye media aliamua kufunga ndoa na Mbunge wa Donge, Sadifa Juma.
Hivi karibuni mahusiano ya wawili hao yamerudi kwenye traki na Bond amekiri kuwa watoto walimpenda sana yeye awe na mama yao kuliko mwaume mwingine "alipokuwa kwenye ndoa, watoto wake walinifuata na kunimbia kuwa hawakufurahishwa mama yao kuolewa na mtu mwingine kwa sababu ya mapenzi ya dhati niliyokuwa nikimuonyesha enzi zile za mahusiano yetu mara ya kwanza." “Upendo wangu ndiyo uliomrudisha Wastara maana niliamua kubadilika na kuachana na pombe kwa ajili yake.
BOND hakuishia hapo pia alitoa angalizo kwa wanawake wanaomfutafuata na kusema " nawaomba wanawake wanaonisumbua kunitaka kimapenzi waache kwani ninaye Wastara, mwanamke wa maisha yangu, siwezi kumsaliti tena, ndani ya mwaka huu tutafunga ndoa,”
No comments:
Post a Comment