MAZISHI ya nguli wa muziki nchini Congo, Papa Wemba, ambaye amepoteza maisha Aprili 24 nchini Ivory Coast, yamesogezwa mbele badala ya kuzikwa leo atazikwa kesho.
Inadaiwa kwamba rais wa nchi hiyo, Joseph Kabila, aliiomba familia ya marehemu, Papa Wemba, kusogeza mbele mazishi hayo kwa ajili ya kuwapa nafasi wadau na marafiki wa marehemu wanaowasili leo nchini humo ili wawahi mazishi hayo.

Baada ya kifo hicho kutokea rais huyo alitoa ndege kwa ajili ya kuchukua maiti jijini Abidjan nchini Ivory Coast hadi Kinshasa.

Kifo cha msanii huyo hadi sasa kimekuwa na utata, huku kukiwa na habari kwamba aliwekewa sumu kwenye kipaza sauti chake na kumfanya apoteze maisha papo hapo baada ya kuanguka jukwaani, uchunguzi wa kifo chake unaendelea.

Papa Wemba kuzikwa kesho


MAZISHI ya nguli wa muziki nchini Congo, Papa Wemba, ambaye amepoteza maisha Aprili 24 nchini Ivory Coast, yamesogezwa mbele badala ya kuzikwa leo atazikwa kesho.
Inadaiwa kwamba rais wa nchi hiyo, Joseph Kabila, aliiomba familia ya marehemu, Papa Wemba, kusogeza mbele mazishi hayo kwa ajili ya kuwapa nafasi wadau na marafiki wa marehemu wanaowasili leo nchini humo ili wawahi mazishi hayo.

Baada ya kifo hicho kutokea rais huyo alitoa ndege kwa ajili ya kuchukua maiti jijini Abidjan nchini Ivory Coast hadi Kinshasa.

Kifo cha msanii huyo hadi sasa kimekuwa na utata, huku kukiwa na habari kwamba aliwekewa sumu kwenye kipaza sauti chake na kumfanya apoteze maisha papo hapo baada ya kuanguka jukwaani, uchunguzi wa kifo chake unaendelea.

No comments:

Post a Comment